Friday, September 21, 2007

Politics Comments on Kass FM 21 Sep 2007

Araap Sang/Mutahi/Araap Magut,
Ahsante kwa sababu ya kiwango ambacho ni cha juu kwani wao ni wale ambao unaweza kuwaita 'matirenik'. Ningependa kusema kwamba kwa wao wanaowania kiti cha rais ya Kenya, watu wanafahamu ni nani hawezi kuaminika tena! Basi ningependa kuwauliza wao maswali mawili tu.

1. Mwaka wa 2002, Kibaki alichaguliwa kwa nguvu za mseto (coalition), baadaye akajaribu kuvunjilia mbali hiyo roho ya kukutanisha vyama. Je, anaporudi sasa kutafuta tena mseto mpya ya Panu, anaweza kuaminika kwa sababu wakati ule alipata kiti akiwa kitandani lakini sasa anaweza kujifanyia kampeni?

2. Kufuatia kuhama kwa Mhe Kenyatta kujiunga na Panu, kuhama kule kuna maanisha nini kwa siasa ya 'baada ya Kibaki' na jee inawezekana kuwa watu kama akina Kombo/Saitoti na wengine wanayo nafasi kweli katika mpangilio huu wa Uhuru/Moi Vs Kibaki (na watu wake wanao panga kuwania wadhifa wa kuongoza) ama wasahau?

No comments:

Search Nandi Kaburwo